Ticker

6/recent/ticker-posts

MUNGU HAKUKUSUDIA WANANDOA WAISHI KAMA WAPANGAJI (Wimbo wa Mama Mchungaji Lawi)

 NDOA - Mama Mchungaji Lawi

MUNGU HAKUKUSUDIA WANANDOA WAISHI KAMA WAPANGAJI

Wakati pekee ambapo katika uumbaji Mungu alisema SI VEMA au HAJAFURAHI ni pale alipoona Adamu ni mpweke. Mwanzo 2:18 “Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.”

Leo tuna wanandoa wengi wanaoishi kama wapangaji – yaani wanaishi pamoja lakini kila mmoja ana mipango yake, malengo yake na maono yake. Hawa wamevaa tu koti la ndoa lakini ni wapweke (married singles).

Mungu anataka ndoa iwasaidie wanandoa kuukabili upweke (married couple) – yaani watoke kwa wazazi (waanzishe mfumo mpya wa maisha yao), waambatane (wawe na mambo yanayowaunganisha) na ndipo watakuwa mwili mmoja (watakamilishana badala ya kutofautiana). Mwanzo 2:24 “Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.”

Msikilize Mwinjilisti Minja (mama Mchungaji Lawi) na timu yake wakisema na wewe.

Kama wanandoa tunashirikiana katika huduma za semina na makongamano kwa vile tunaamini ndoa ni wajibu mkubwa katika ufalme wa Mungu na sio nyumbani peke yake. Wasiliana nasi.  

Kumbuka ku-follow ukurasa na ku-subscribe kwenye channel yetu.

Dkt. Lawi Mshana, +255712924234, Korogwe, Tanga, Tanzania