Ticker

6/recent/ticker-posts

Tambua na kuitumia vizuri neema katika maisha yako

TAMBUA NA KUITUMIA VIZURI NEEMA 

KATIKA MAISHA YAKO

Maono: Nilisikia ujumbe ukisema, Neema inatufundisha kukataa ubaya. (Ikabidi nilitafute hili andiko na kulisoma vizuri)

Tito 2:11-15 “Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa12 nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; 13 tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;14 ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.15 Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote.”

 Vipengele vya maombi

1. Neema ya wokovu ifunuliwe kwetu – Hii neema ni zaidi ya kusema, Nimeokoka. Neno ‘wokovu’ limebeba mambo mengi (holistic) kv wokovu wa roho, uponyaji, mafanikio, kurejezwa, kuhuishwa nk. 2 Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.” 

2. Tufundishwe kukataa ubaya (ungodliness) na tamaa za dunia (wordly lusts) – tuwe na tabia za Uungu. 2 Petro 1:4 “Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.” 

3. Tuwezeshwe kuishi kwa kiasi (soberly), haki (righteous) na utauwa katika ulimwengu huu wa sasa (godly in the present age)

Tito 3:14 “Watu wetu nao wajifunze kudumu katika matendo mema, kwa matumizi yaliyo lazima, ili wasiwe hawana matunda.”

4. Tuweze kutazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu 

1 Yohana 3:2,3 “Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu.”

5. Tutambue kazi ya Yesu msalabani (kujitoa kisadaka, kutukomboa na maasi yote, kutusafisha tuwe milki yake [wenye juhudi katika matendo mema] )

 Ebr 12:2 “tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.”

6. Tuwe jasiri na kujituma katika utumishi bila kuogopa watu 

2 Timotheo 2:1 “Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu.” Mithali 29:25 “Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye Bwana atakuwa salama.”

Lawi Mshana, +255712924234, Tanzania