Ticker

6/recent/ticker-posts

MWALIKO WA KIPINDI CHA WATOTO/VIJANA WA DINI ZOTE


 MWALIKO WA KIPINDI CHA WATOTO/VIJANA WA DINI ZOTE

Washiriki: Watoto na vijana (adolescents and youth) kuanzia umri wa miaka 10 hadi 24

Wapi: Ukumbi wa Hema (TLMC) karibu na Magereza – Manundu kati (Korogwe mjini)

Lini: Jumapili tarehe 25 Juni 2023

Muda gani: Saa 9.30 alasiri

Mada: Stadi za maisha za kushinda vishawishi na uhatarishi

Kwanini: Watoto na vijana wanakabiliwa na changamoto nyingi nyumbani, mtaani wakienda na kutoka shule, shuleni, mtandaoni na wanapotembelea jamaa na marafiki.

Waandaaji: Nitatoboa Initiative (mpango wa malezi ya vijana balehe na vijana wadogo) unaoratibiwa na shirika la Beyond Four Walls, Korogwe, Tanga.

Mzazi na mlezi tunakuomba umruhusu kijana ashiriki kipindi hiki ili kumlinda dhidi ya changamoto nyingi zinazomkabili ukizingatia ni kipindi cha likizo na ni wikiendi.

Beyond Four Walls ni shirika lisilo la kiserikali linalojengea uwezo jamii ishinde uhatarishi, utegemezi na umasikini kwa kutumia mbinu shirikishi.

“We look at Tanzanian youth as potential partners, rather than just as beneficiaries.”