Ticker

6/recent/ticker-posts

BADO JAMII HAITAMBUI UZITO WA KAZI YA WALIMU NA WAHUDUMU WA AFYA


 BADO JAMII HAITAMBUI UZITO WA KAZI YA WALIMU NA WAHUDUMU WA AFYA

Leo tulikuwa na muda wa kupitia matokeo ya tathmini ya awali kwenye shule ya sekondari ambayo wanafunzi wake walishiriki katika mahojiano hapa Dodoma Jiji. Tulithibitisha uhatarishi uliotajwa na wanafunzi ili tujue namna tutakavyotafuta ufumbuzi wa kudumu.

Lakini walimu pia wana changamoto nyingi. Jamii inamtarajia mwalimu afanye zaidi ya matarajio bila kujali kwamba na yeye ana mahitaji ya msingi katika kuboresha mazingira yake ya kazi na ya familia. Hakuna wakati mwalimu akikosea anachukuliwa kama ni bahati mbaya. Pamoja na kujitolea kufundisha muda wa ziada bila malipo, bado jamii haitambui kwamba amejitolea. Mwalimu anaweza kufokewa mbele za watu bila sababu za msingi.

Tunahitaji kuwajali walimu tukizingatia kwamba wana muda mwingi na watoto wetu kuliko sisi wenyewe kama wazazi.

Ungana nasi katika mpango wetu wa kutambua kazi njema wanayofanya walimu na wahudumu wa afya kama makundi ambayo jamii inaona mapungufu yao tu na kusahau mazuri wanayoyafanya.

Dr Lawi Mshana, Beyond Four Walls, 0712-924234