Ticker

6/recent/ticker-posts

SIKU YA TATU YA ZIARA YETU YA KUTHIBITISHA UHATARISHI SHULENI – DODOMA JIJI


SIKU YA TATU YA ZIARA YETU YA KUTHIBITISHA UHATARISHI SHULENI – DODOMA JIJI

Tunashukuru sana kwa ushirikiano mkubwa ambao tumeendelea kuupata kutoka kwa walimu wakuu na walimu waliokaa kikao na sisi. Naamini baada ya zoezi hili tutakuwa tumepata uhalisia wa changamoto ambazo ziko ndani ya uwezo wa shule na zile ambazo zinahitaji kuungwa mkono na wadau wengine katika kuzitatua.

Tunaamini walimu pia wana changamoto nyingi ambazo zinahitaji kupatiwa ufumbuzi. Kuna wakati tunasahau kwamba hata walimu wanatoka katika familia hivyo wanahitaji pia malezi na matunzo.

Ungana nasi katika huduma hii ukizingatia kwamba watoto wetu wako muda mwingi zaidi shuleni kuliko nyumbani na katika nyumba za ibada.

Dr. Lawi Mshana, Beyond Four Walls NGO, +255712924234