Ticker

6/recent/ticker-posts

KIKAO CHA ‘KIKOSI KAZI’ CHA KUANDAA MKAKATI WA KUKABILIANA NA UHATARISHI - DODOMA





KIKAO CHA ‘KIKOSI KAZI’ CHA KUANDAA MKAKATI WA KUKABILIANA NA UHATARISHI - DODOMA

Katika kikao chetu cha kutoa matokeo kuhusu ripoti ya tathmini ya awali (needs assessment report) tulikubaliana tuwe na kikosi kazi chenye wajumbe kutoka kila mtaa kwenye kata tunayofanya kazi hapa Jijini Dodoma.

Leo tumekutana kuthibitisha uhatarishi ulioainishwa na kuweka mkakati wa namna tutakavyoukabili tukishirikiana na serikali na wadau wa maendeleo. Lakini pia tumeanza kukutana na walimu kwa ajili ya mkakati wa kufanya kazi pamoja kukabili uhatarishi mashuleni.

Tunahitaji sana msaada wako wa kuunga mkono juhudi hizi ili vijana balehe na vijana wa nje ya shule wawe salama shuleni, njiani, nyumbani na katika nyumba za ibada.

Wasiliana nasi sasa!

Dr Lawi Mshana, Beyond Four Walls, 0712924234 (Simu na Whatsapp)