Ticker

6/recent/ticker-posts

MUNGU AKINUFAIKA NA WEWE, ANAJIBU HARAKA MAHITAJI YAKO BINAFSI

MUNGU AKINUFAIKA NA WEWE, ANAJIBU HARAKA MAHITAJI YAKO BINAFSI

Usiku tukiwa katika maombi nilipata ujumbe huu muhimu kwako unayetafuta sana upendeleo (favor) wa Mungu. Tatizo lako unaombea na kutafuta sana ufumbuzi wa mahitaji yako ya kibinafsi na kusahau kuombea mambo ambayo yanamgusa Mungu kwa haraka. Ukimgusa Mungu hawezi kuacha kutimiza mahitaji yako hata kama hujamuomba. Hebu jiulize: Hivi Rais wa nchi yetu akiona unamfaa, utakuwa na ulazima wa kumueleza shida zako binafsi?

1. Tafuta mafanikio ya kazi ya Mungu kuliko ya kwako binafsi

Maandiko yameweka wazi kwamba kama unataka KUZIDISHIWA (kujibiwa mahitaji yako binafsi), UTAFUTE KWANZA UFALME WA MUNGU NA HAKI YA MUNGU.

Mathayo 6:33 “Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.”

2. Usijisumbue sana na kusahau kwamba Mungu ndiye aliamua kukuleta duniani

Usijisumbue (usi-struggle) sana na maisha bali jifunze kujikabidhi kwa Bwana alliyekuleta hapa duniani kwa kusudi maalum. Anajua kwa nini alikuleta duniani. Wafilipi 4:6 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.”

3. Hana alipata watoto wake mwenyewe baada ya kuamua kuomba kwanza apewe mtoto kwa ajili ya kazi ya Mungu.

Alipozomewa kwa kutozaa alifika mahali akaamua aombe mtoto ambaye hatanufaika naye.

1 Sam 1:11 “Akaweka nadhiri, akasema, Ee Bwana wa majeshi, ikiwa wewe utaliangalia teso la mjakazi wako, na kunikumbuka, wala usinisahau mimi mjakazi wako, na kunipa mimi mjakazi wako mtoto mume, ndipo mimi nitakapompa Bwana huyo mtoto siku zote za maisha yake, wala wembe hautamfikilia kichwani kamwe.”

Baada ya kumpata mtoto huyo ndipo tumbo lake likafunguka kwa ajili ya watoto wake binafsi. 1 Sam 2:21 “Naye Bwana akamwangalia Hana, naye akachukua mimba, akazaa watoto, wa kiume watatu na wa kike wawili. Naye huyo mtoto Samweli akakua mbele za Bwana.”

Mungu ana majibu yako lakini ufunguo wake ni kuhakikisha unatanguliza ufalme wa Mungu kuliko maisha yako binafsi. Tangu wengine tugundue siri hii hatujapungukiwa.

Mwaliko

Tunajiandaa kumaliza mwaka na kuanza mwaka mwingine. Huduma tunayofanya inagusa na kujengea uwezo jamii bila kubagua dini wala dhehebu. Tunakualika uungane nasi kwa kujaza fomu ya kujitolea kuwa rafiki-mwenza au mdau (partner) kwa mwaka 2025. Zipo huduma unazoweza kuzifanya hata kama uko mbali nasi. Shiriki katika maono haya makubwa yanayogusa ulimwengu mzima. Yapo mataifa ambayo haingekuwa rahisi kuyafikia lakini kupitia huduma hii tumeweza kuyafikia.

Njia rahisi zaidi ni kuwasiliana nasi ni kwa kupitia hapa kwenye tovuti (WASILIANA NASI) au baruapepe (info@lawimshana.com) au kupitia Whatsapp (0712-924234).

Wewe ni mtu muhimu sana kwetu.

Karibu sana

0712924234.