Ticker

6/recent/ticker-posts

Karibu ushiriki maombezi kwa wasap bure


Video: Karibu ushiriki maombezi kwa wasap bure

MWONGOZO WA KIPINDI CHA KLINIKI YA UPONYAJI

KITUONI NA MTANDAONI

Dr. Lawi Mshana

Kliniki ya uponyaji ni kipindi cha maombezi nje ya muda wa ibada za Kanisa ambacho ni maalum kwa ajili ya watu wenye matatizo sugu ambayo yana udhihirisho wa wazi wa nguvu za giza.

Mtu anapohitaji huduma hii anapaswa kufanyiwa mahojiano ya kutambua uzito wa tatizo lake (diagnosis) na awe tayari kushiriki vipindi kadhaa mpaka atakapokuwa huru kwelikweli. Kuna wakati Mungu haponyi kwa MUUJIZA wa papo kwa papo bali anaponya kwa MCHAKATO (HATUA KWA HATUA). Anayefanyiwa huduma ataeleza mabadiliko anayoyapata mpaka atakapofunguliwa.

Andiko linaloongoza Kliniki ya Uponyaji ni Mk 8:22-26 “22 Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse. 23 Akamshika mkono yule kipofu, akamchukua nje ya kijiji, akamtemea mate ya macho, akamwekea mikono yake, akamwuliza, Waona kitu? 24 Akatazama juu, akasema, Naona watu kama miti, inakwenda. 25 Ndipo akaweka tena mikono yake juu ya macho yake, naye akatazama sana; akawa mzima, akaona vyote waziwazi. 26 Akampeleka nyumbani kwake, akisema, Hata kijijini usiingie.”

Andiko hilo linatufundisha kwamba kuna matatizo ambayo Mungu hayaondoi kwa TUKIO la muujiza wa papo kwa papo bali kwa MCHAKATO.

Kuna mambo kadhaa ambayo yalifanyika kabla ya huyu mtu kuwa huru kwelikweli.

1. Yesu alimtoa nje ya kijiji – alimtoa katika mazingira hatarishi

2. Yesu alimwekea mikono – alimfanyia huduma ya uponyaji

3. Yesu alimuuliza kama anaona kitu – alitaka kujua mabadiliko yaliyoanza kutokea

4. Yule mtu alitazama juu – alifanyia kazi kile alichokuwa hawezi ili agundue kama amepona

5. Yule mtu alisema anaona watu kama miti inayotembea – alieleza hali yake bila kuficha (alisema amepata nafuu ila bado hajapona vizuri). Hakulazimishwa kukiri kwamba amepona.

6. Yesu alimuwekea tena mikono yake – alipoona kwamba hajapona vizuri alimgusa tena

7. Yule mtu alitazama sana akaona vizuri – alijitahidi kufanya anachoweza ili kuthibitisha kama amepona ndipo akapona kabisa

8. Yesu hakumruhusu kuingia kijijini – hakuruhusiwa kurudi kwenye kile kijiji (pengine kilikuwa na maagano yaliyosababisha matatizo yake)

Kwa yule ambaye anaweza kufika katika kituo chetu anapaswa kuzingatia mambo yafuatayo:

1. Afanyiwe mahojiano ili kugundua uzito wa tatizo lake – matatizo mengine yanahitaji aombewe kwenye vipindi vya maombi vya kanisa au kwenye kikundi cha maombi. Hata hivyo lazima mhitaji (mteja) apangiwe muda maalum (appointment) kwa vile ni huduma inayohitaji kuombea kwa ufuatiliaji wa karibu na sio kuombea kundi la watu kwa pamoja.

2. Kama ana sifa za kufanyiwa maombi katika kipindi cha Kliniki ya Uponyaji atatakiwa kufanya yafuatayo:

·       Atatakiwa kushiriki kipindi cha maombezi ya ufunguzi cha Jumatatu saa 4 asubuhi – kipindi hiki kimepangwa muda huu wa asubuhi kwa sababu zifuatazo: Kuhudumia mhitaji aliyechoshwa na tatizo lake kiasi cha kusimamisha kazi zake kama anavyofanya anapoenda hospitali, muda huu atahudumiwa akiwa bado hajachoshwa na kazi zake binafsi, tutakuwa na muda wa kutosha kuombea, kuhoji na kushauri kuliko jioni, ni muda wenye utulivu mkubwa kwa vile hata wanafunzi wako mashuleni, hauingiliani na ibada za makanisani na wahitaji wanaotoka mbali wataweza kuja na kurudi kila siku bila kikwazo.

·       Atatakiwa kuwa tayari kufululiza kwa siku kadhaa (hata hivyo baada ya siku ya kwanza muda unaweza kubadilika kulingana na aina ya tatizo na nafasi ya wahudumu.)

     Atafanyiwa huduma katika maeneo makuu manne – 1. Uponyaji wa ndani

     2. Kuangusha ngome 3. Kuondoa haki ya kisheria ya mapepo 4. Kutoa mapepo

3. Mhitaji atatakiwa kusindikizwa na ndugu wa karibu ili kusaidia dharura zikijitokeza (hasa kwa wenye mapepo au magonjwa yanayohitaji usaidizi wa karibu). Sio lazima huyo msaidizi wake ahusike katika vita vya kiroho. Anaweza kuwa nje na kuitwa pale dharura inapojitokeza.

4. Mhitaji asije na mtoto mdogo (amuachie mtu mwingine) – ni hatari kuwa katika vita ukiwa na watoto (ikibidi aje na msaidizi atakayekaa na mtoto huko nje). Mtoto anaweza kuathirika kisaikolojia anapoona mapepo yanavyomtesa mzazi wake. Lakini pia huduma haitafanyika katika utulivu kama kuna watoto wadogo.

5. Mhitaji avae nguo za kujisitiri ili kama ana mapepo yasimdhalilishe – Tunapendekeza kama ni mwanamke avae gauni refu ambalo halijambana badala ya sketi na blauzi. Mwanaume pia avae suruali ambayo haijambana sana.

6. Mhitaji ajiandae maji yake ya kunywa na kujihudumia kwa chakula na mahitaji mengine binafsi. Kuna nyumba za wageni na mgahawa karibu na kanisa. - Huduma hii inatolewa bure na hatuuzi vifaa vyovyote kv maji, mafuta na vitambaa. Bwana aliyetupa huduma hii ametuonya tusiwatoze watu tunapowahudumia. Mathayo 10:8 “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.”

7. Kuna wakati huduma hii inafanyika kwa njia ya mtandao (kukitokea dharura) kv Whatsapp meeting calls, Zoom, Google meet nk.

Ratiba inaweza kubadilika kutokana na dharura za huduma zingine au safari. Hivyo wasiliana na wahudumu wakujulishe kama kuna mabadiliko yoyote.

Tuko Korogwe mjini karibu na Magereza kando ya barabara ya Maembe kwenda NSSF. Utaona kanisa la Transformed Life Mission Church (TLMC).

KWA WANAOTAKA KUSHIRIKI KWA NJIA YA MTANDAO

Unaweza kushiriki vipindi kwa njia ya mtandao au kupewa appointment ya kuombewa kwa njia ya mtandao.

Kwa mwenye Whatsapp unaweza kunijulisha majina yako, ulipo, mahitaji yako, maelezo machache ya hatua ulizowahi kuchukua na matokeo uliyopata, muda na siku ambazo unaweza kushiriki nk.

Hakikisha ume-save namba yangu ya simu na whatsap yako ina picha yako ndipo itakuwa rahisi kukutumia kiungo (link) ili ushiriki. Usisahau kujiunga kifurushi cha mtandao wa simu ambao una nguvu hapo ulipo ili mawasiliano yasikatikekatike. Tutatumia zaidi ‘audio’ badala ya ‘video’ ili hata wenye mtandao dhaifu waweze kushiriki. Kumbuka kuzima mic (mute) hadi pale unapopewa nafasi ya kuongea. Itasaidia kelele za mahali ulipo zisiathiri huduma inayoendelea mtandaoni.

Kumbuka: Atakayepokea ujumbe wa kushiriki huduma ya mtandaoni kwa whatsap ni yule tu aliye-save namba yangu kwenye simu yake. Lakini pia kuna ukomo wa idadi maalum ya washiriki.

Kama watakuwepo washiriki wasiojua Kiswahili, tutachanganya na lugha ya Kingereza ili nao wasiachwe kabisa.

Unaweza kupata maelekezo zaidi kupitia kupitia tovuti ya www.lawimshana.com (Faith and Community Empowerment). Nenda kwenye “Google search” uandike Lawi Mshana, utaipata hii tovuti. Pia ndani ya Tovuti utaona DOWNLOAD APP ambapo utapata App ya ‘Faith Empower’ ili kupata huduma zote sehemu moja (all-in-one platform).

Kwa unayetaka kushiriki kipindi hiki kituoni, wasiliana nasi kupitia simu hizi: 0657-705509; 0775-591345; 0693-925055

Kwa huduma ya Kliniki ya Uponyaji mtandaoni wasiliana nami kwa Whatsapp kupitia 0688-986882.

Dr. Lawi Mshana, Tanzania