Jibu
1. Tutambue milango iliyosababisha shetani
akapata nafasi na kisha tuifunge. Mfano, marafiki wabaya, sherehe mbaya,
vijiwe, kazi zisizofaa nk
Waefeso 4:27 “wala msimpe Ibilisi nafasi.”
1 Petro 5:8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama
simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.” Kutoka 34:15 “Usije ukafanya agano na wenyeji wa
nchi, watu wakaenda kufanya uzinzi na miungu yao, na kuitolea sadaka miungu
yao; mtu mmoja akakuita, ukaila sadaka yake.” Mf marafiki, vijiwe, kazi nk
2. Tufanye kitu fulani kwa ajili ya Mungu KILA
SIKU (sio kila ibada) – mapepo yanarudi kama baada ya kutolewa yamekuta nafasi
ni tupu (hujampa Yesu nafasi atawale maisha yako).
Luka 11:24-26 “Pepo mchafu amtokapo mtu,
hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika; asipoona, husema,
Nitairudia nyumba yangu niliyotoka. Hata afikapo, akaiona imefagiwa na
kupambwa, ndipo huenda akachukua pepo wengine saba, walio waovu kuliko yeye mwenyewe,
wakaingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya
kwanza.”
3. Tuepuke ibada za shetani na watu wenye maagano
na shetani – hakikisha unaabudu mahali sahihi. Usiwekewe mikono na mawakala wa
shetani na usitoe sadaka mahali ambapo sadaka yako inapelekwa kwenye madhabahu
za shetani. Kuna makanisa ambayo waumini wanatolewa kafara kila mwaka.
Kum 12:14 “bali katika mahali atakapopachagua
Bwana katika kabila zako mojawapo, ndipo utakapotoa sadaka zako za kuteketezwa,
ndipo utakapotenda yote nikuamuruyo.” 2 Wakorintho 6:17 “Kwa hiyo,
Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami
nitawakaribisha.” 1 Wakorintho 5:11 “Lakini, mambo yalivyo,
naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au
mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang'anyi;
mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.”
4. Tujitiishe kwa Mungu na kumpinga shetani –
shetani hawezi kukimbia kama unayemkemea huna uhusiano wa karibu na Mungu. Ukijaribu
kumkemea wakati huna sifa anaweza kukuaibisha.
Yakobo 4:7 “Basi mtiini Mungu. Mpingeni
Shetani, naye atawakimbia.”
Mdo 19:13-16 “Baadhi ya Wayahudi wenye
kutanga-tanga, nao ni wapunga pepo, wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu
yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nawaapisha kwa Yesu, yule
anayehubiriwa na Paulo. Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi,
kuhani mkuu, waliofanya hivyo. Yule pepo mchafu akawajibu, akawaambia, Yesu
namjua na Paulo namfahamu, lakini ninyi ni nani? Na yule mtu aliyepagawa na
pepo mchafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio
katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.”
5. Tufunge na kuomba mara kwa mara – kuna mambo
hayawezi kufanyika bila kufunga na kuomba. Hata hivyo usifunge (usishinde njaa)
wakati huna muda wa kuomba. Hata wajumbe wa shetani wanafunga ili kupata nguvu
za kiroho. Wanafunga hata siku 14. Je, wewe si zaidi?
Mathayo 17:19-21 “Kisha wale wanafunzi
wakamwendea Yesu kwa faragha wakasema Mbona sisi hatukuweza kumtoa? Yesu
akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia,
Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa
uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu. Lakini
namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.”
Sababu ziko nyingi. Hebu ongeza zingine unazozikumbuka hapo chini kwenye POST A COMMENT.
Dr. Lawi Mshana, Freelance Facilitator
& Public Speaker, 0712924234, Tanzania