Ticker

6/recent/ticker-posts

Wasamaria wema wamenusuru maisha ya mama na mtoto



 WASAMARIA WEMA WAMENUSURU MAISHA YA MAMA NA MTOTO

Baada ya kupata mafunzo ya kukabiliana na majanga na kisha kuunda kamati ya usimamizi, tumeweza kuhusika kumnusuru mama aliyepata uchungu akiwa katika mazingira magumu. Alipata uchungu na akawa hana nauli hata ya bajaji wala msaidizi yeyote nyumbani kwake. Tuliwapata wasamaria wengine walioungana nasi kutoa mahitaji mbalimbali kama vile nauli ya kumkimbiza hospitalini, ndoo, nguo za mama na za mtoto mchanga, chandarua cha mtoto na nauli za kumpeleka kijijini kwa wazazi wake ili akapate uangalizi wa karibu baada ya kujifungua salama. Wapo majirani waliokubali kuchukuliwa ghafla wakiwa njiani ili wamsindikize hospitalini. Hata hivyo kwa mujibu wa kitengo chetu kazi bado haijaisha. Anahitaji elimu zaidi atakaporudi ili kupunguza uwezekano wa tatizo hili kujitokeza katika hali ya uhatarishi kiasi hicho.

Unaweza kuungana nasi kama Msamaria mwema wa kusaidia watu wanapopata majanga, kusaidia kupunguza uwezekano wa majanga kutokea, kusaidia kuponya kiroho na kihisia watu waliopata majanga nk.

Bilashaka unazo nguo na vitu mbalimbali ambavyo viko nyumbani kwako kwa sasa na huvitumii kwa vile Mungu amekusaidia kupanda hatua nyingine ya maisha. Pamoja na kwamba unayo pia mahitaji mengine, naomba Mungu akupe moyo wa kutupatia vitu hivyo ili tuweze kutoa misaada ya dharura majanga yanapotokea. Tutakutambua kama mshirika (partner) au ambassador (balozi) wa kushirikiana na Beyond Four Walls katika kushughulika na uhatarishi na majanga yanayotokea katika jamii.

Pia unaweza kujiunga na group letu jipya la Vulnerability & Disaster Management (USIMAMIZI WA UHATARISHI NA MAJANGA) ambalo liko Facebook na Whatsapp.

ANGALIZO: Beyond Four Walls sio shirika la kutoa misaada bali kuhamasisha na kujengea uwezo jamii katika kukabiliana na uhatarishi na majanga kwa kutumia mbinu shirikishi. Kwa ushirikiano wako tutaifikia jamii nzima ya Kitanzania hatua kwa hatua.

Lawi Mshana, 0712-924234