Ticker

6/recent/ticker-posts

FAHAMU MAPENZI YA MUNGU KWAKO (Soma maandishi na kuangalia video fupi)

FAHAMU MAPENZI YA MUNGU KWAKO (Bofya hapa uangalie video)

FAHAMU MAPENZI YA MUNGU KWAKO 

Kila mmoja wetu amewekwa hapa duniani kwa kusudi maalum. Ndiyo maana alama za vidole gumba hazifanani. Hivyo si mpango wa Mungu uwe fotocopi ya mtu fulani. Utapata tabu sana kama hujui mapenzi ya Mungu kwako.

Mungu anaweza kuruhusu maisha fulani kwako kwa sababu fulani.

Waefeso 5:10 “mkihakiki ni nini impendezayo Bwana.(finding out what is acceptable to the Lord)” Waefeso 5:17 “Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.”

1 Yohana 5:14 “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.”

Tunawezaje kuyajua mapenzi ya Mungu

1. Kusoma na kuelewa Neno Lake

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.”

Zaburi 119:105 “Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.”

Neno linalokujia kwa uvuvio bila kupingana na maandiko matakatifu (Neno la Bwana likanijia kusema…). Hakuna andiko linalotaja umuoe fulani au uolewe na fulani. Ila huwezi kupewa neno la kuoa mke wa mtu, kuishi bila utaratibu nk.

2. Kugeuzwa kwa kufanywa upya nia (mindset) = metamorphosed

Rum 12:2 “Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.”

3. Kumuomba Mungu na kumsubiri

Luka 22:42 “akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke.”

Mfano: Paulo: 2 Kor 12:7-10 “Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi. Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke. Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.”

Maombi ya wiki hii:

1. Ee Mungu naomba unipe neno la kinabii la kuniongoza katika maisha yangu ili nisitafute maisha ambayo hujanipangia.

2. Ee Mungu naomba unifundishe kuomba na kuwa na subira ili nisipishane na majibu yako.

3. Ee Mungu naomba usafishe akili yangu ili niweze kujua mapenzi yako kwangu.