Ticker

6/recent/ticker-posts

JISHUSHE NA KUFURAHIA MAENDELEO YA WENGINE (VIDEO NA MAANDISHI)

JISHUSHE NA KUFURAHIA MAENDELEO YA WENGINE (Bofya uangalie video)

JISHUSHE NA KUFURAHIA MAENDELEO YA WENGINE

Usipende kuonekana unajua kila kitu. Uwe na roho ya kujifunza kwa wengine bila unafiki.

Wafilipi 2:3,5-8 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. 5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;  6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;  7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; 8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

Mwanzo wa anguko ni kuwa na kiburi

Mit 16:18 “Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.”

Ujuzi huleta majivuno

1 Kor 8:1,2 “Na kwa habari ya vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu; Twajua ya kuwa sisi sote tuna ujuzi. Ujuzi huleta majivuno, bali upendo hujenga. Mtu akidhani ya kuwa anajua neno, hajui neno lo lote bado, kama impasavyo kujua.”

Unapooona umefanikiwa, jisifu ndani ya nafsi yako mwenyewe

Gal 6:3,4 “Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake. Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake.”

Mfano mzuri wa kujifunza unyenyekevu

Mt 3:11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.”

Yohana hakukasirika Yesu alipomchukulia washirika na kupata umaarufu kuliko yeye. Alijitambua Yeye ni nani na mipaka ya huduma yake. Yn 3:26-30 “Wakamwendea Yohana, wakamwambia, Rabi, yeye aliyekuwa pamoja nawe ng'ambo ya Yordani, yeye uliyemshuhudia, tazama, huyo anabatiza na watu wote wanamwendea. Yohana akajibu, akasema, Hawezi mtu kupokea neno lo lote isipokuwa amepewa kutoka mbinguni. Ninyi wenyewe mwanishuhudia ya kwamba nalisema, Mimi siye Kristo, bali nimetumwa mbele yake. Aliye naye bibi arusi ndiye bwana arusi; lakini rafiki yake bwana arusi, yeye anayesimama na kumsikia, aifurahia sana sauti yake bwana arusi.  Basi hii furaha yangu imetimia. Yeye hana budi kuzidi, bali mimi kupungua.”

Yn 21:17,20-22 “Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu. Petro akageuka akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu anafuata; (ndiye huyo aliyeegama kifuani pake wakati wa kula chakula cha jioni, akasema, Bwana, ni nani akusalitiye?) Basi Petro akamwona huyo, akamwambia Yesu, Bwana, na huyu je? Yesu akamwambia, Ikiwa nataka huyu akae hata nijapo, imekupasaje wewe? Wewe unifuate mimi.”

Petro hakuridhika na kazi aliyopewa. Akataka kujua mambo yasiyomhusu.

2 The 3:11 “Maana twasikia kwamba wako watu kwenu waendao bila utaratibu, hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha na mambo ya wengine.” – uwe na shughuli zako mwenyewe

Maombi ya wiki hii:

1. Ee Mungu naomba uniondolee roho ya kiburi ili niwathamini wengine na kuweza kujishusha.

2, Ee Mungu naomba uniwezeshe kukuinua kupitia mafanikio yangu ili uzidi kujitukuza kupitia maisha yangu.

Napenda kuwashukuru wote ambao mwaka huu mliguswa kuchangia huduma hii hata nikaweza kuandaa masomo na kuyatuma mtandaoni bila malipo yoyote. Nawahakikishia kwamba siku ya mwisho tutagawana thawabu maana bila mchango wenu singeweza peke yangu kuwafikia watu wengi bila tozo yoyote.
Tayari fomu ziko tayari kwa ajili ya ahadi za kila mwezi au kila robo mwaka za mchango wako wa hiari kwa mwaka 2024. Unapoahidi unaniwezesha kuwa na mpango maalum wa kuifikia jamii na kupata vitendea kazi kwa ajili ya huduma kwa jamii bila mipaka ya kidini na kimadhehebu.
Wasiliana nami ili upatiwe fomu ambayo itakuwezesha kuchangia kwa fedha zako, ujuzi wako, vipawa vyako, muda wako na nguvu zako. Kuanzia tarehe 1 Januari ni muda wa kuwakabidhi kwa Mungu marafiki (partners) wanaochangia huduma hii ili neema nyingi iwe juu yao.
Mathayo 10:41 "Ampokeaye nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; naye ampokeaye mwenye haki kwa kuwa ni mwenye haki, atapata thawabu ya mwenye haki."

Dr. Lawi Mshana, +255712924234; Tanzania