Ticker

6/recent/ticker-posts

FAHAMU MAANA YA KIFO CHA ROHO (Video na maandishi)

FAHAMU MAANA YA KIFO CHA ROHO (Bofya hapa uangalie video)

FAHAMU MAANA YA KIFO CHA ROHO

Kifo kiko kwa namna mbili: Kifo cha kimwili na kifo cha kiroho. Kifo cha kiroho kinaweza kutokea ukiwa bado unatembea duniani na baada ya kuondoka duniani (kutengwa na Mungu milele).

Hata hivyo kuna watu wamezikwa kimwili lakini bado tarehe ya kifo walichopangiwa na Mungu haijafika. Hivyo wanatangatanga wakitumwa kutesa watu (misukule) hapa duniani. Lakini wapo pia watu tunaowaona kimwili lakini ni watumwa wa kuwanufaisha watu fulani (ndondocha). Muda mwingi wanachoka kwa vile wanatumikishwa bila kujua.

Ezekieli 13:19 “Nanyi mmeninajisi kati ya watu wangu, kwa ajili ya makonzi ya shayiri na vipande vya mkate, ili kuziua roho za watu ambao haiwapasi kufa, na kuzihifadhi hai roho za watu ambao haikuwapasa kuwa hai, kwa kuwaambia uongo watu wangu wasikilizao uongo.”

Shetani anaweza kuua mwili wako lakini baada ya hapo hawezi lolote tena.

Mathayo 10:28 “Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum.”

Ili kuwa salama baada ya maisha haya lazima kuzaliwa mara ya pili (kuzaliwa kiroho)

Yohana 3:4-8  Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa? Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu. Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho. Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili. Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho.

Kiungo kimoja cha mwili wako kinaweza kukupeleka Jehanum

Mathayo 18:9 “Na jicho lako likikukosesha, ling'oe, ukalitupe mbali nawe; ni afadhali kuingia katika uzima una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum ya moto.”

Marko 9:43 “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima u kigutu, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika.”

Marko 9:45 “Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum.”

 Kama huishi na kuenenda kwa Roho Mtakatifu, uko hatarini

Warumi 8:13 “kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.” 

Gal 5:25,26 “Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.”

Maombi ya wiki hii:

1. Ee Mungu naomba unipe maisha mapya ili nisiendelee kutumikishwa na shetani.

2. Ee Mungu naomba unipe ushindi wa dhambi na kuniongoza kwa Roho wako ili nisije nikapotea milele.

Lawi Mshana, 0712-924234 (ushauri na maombezi kwa njia ya mtandao).