Ticker

6/recent/ticker-posts

LEO TUMEALIKWA KUFUNDA WANAFUNZI WA SEKONDARI KUHUSU ELIMU RIKA



 LEO TUMEALIKWA KUFUNDA WANAFUNZI WA SEKONDARI KUHUSU ELIMU RIKA

Nashukuru uongozi wa shule ambao umeona umuhimu wa kunialika kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu afya ya uzazi na kushinda unyanyasaji wa kingono ambao umekithiri mashuleni.

Tuko katika kipindi ambacho wanafunzi wako katika uhatarishi mkubwa kwa sababu mkazo mkubwa ni katika ufaulu wa masomo ya kitaaluma tu bila kuwasaidia wanafunzi wajitambue na kupata stadi za maisha za kukabiliana na changamoto za maisha. KUNA MAKATAZO MENGI LAKINI HAKUNA MBINU ZA KURAHISISHA UTEKELEZAJI WAKE!

Kadiri Mungu atakavyotujalia hatutaishia kwa wanafunzi bali tutawafikia pia walimu, wazazi na viongozi wa dini. Wazazi tunakagua zaidi madaftari lakini hatukagui maeneo mengine ya maisha ya watoto wetu. Mpaka tukiona mtoto anachechemea ndipo tunafuatilia na mara nyingi tunakuwa tumeshachelewa sana. Tunapenda kuwasaidia watoto na wazazi wavunje ukimya na kuweza kujadili kuhusu afya ya uzazi na watoto wao bila aibu. Mtoto asipoweza kutuuliza sisi kama chanzo sahihi cha taarifa, atauliza marafiki zake na mitandao ya kijamii na kukutana na upotoshaji.

Ombea na kuwezesha huduma hii kadiri unavyojaliwa ili tukinusuru kizazi chetu na majanga yanayoepukika.

Dr Lawi Mshana, 0712-924234