Ticker

6/recent/ticker-posts

Roho ya kutangatanga haitakutesa tena (Video na Maandishi)

ROHO YA KUTANGA-TANGA HAITAKUTESA TENA  (Bofya hapa uangalie video)

ROHO YA KUTANGA-TANGA HAITAKUTESA TENA

Ndoto: Hivi karibuni niliona nikiwaombea watu kwamba roho ya kutangatanga iwaachie.

1. Katika kuabudu kwako

Mungu anakwenda kukutoa kwa wachungaji waliokufanya chakula chao

Ezekieli 34:6,10 “Kondoo zangu walitanga-tanga katika milima yote, na juu ya kila kilima kirefu; naam, kondoo zangu walitawanyika juu ya uso wote wa dunia; wala hapakuwa na mtu aliyewaulizia, wala kuwatafuta. Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu ya wachungaji; nami nitawataka kondoo zangu mikononi mwao, nami nitawaachisha hiyo kazi ya kuwalisha kondoo; nao wachungaji hawatajilisha wenyewe tena; nami nitawaokoa kondoo zangu vinywani mwao, wasiwe tena chakula chao.”

2. Katika kufikiri kwako

2 Timotheo 3:8 “Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani.”

3. Katika kazi zako

Mungu anakwenda kuondoa laana ya kutanga-tanga ndani yako – hata ukihama miji, sehemu za kazi na kubadili biashara hufanikiwi

Mwanzo 4:12 “utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.”

Sasa ufanyeje?

1. Unatakiwa kujihoji na kumrudia Mungu – tunasikiliza zaidi utabiri wa hali ya hewa kuliko manabii wa Bwana.

Amosi 4:7,8 “Tena nimeizuia mvua msiipate, ilipobaki miezi mitatu kabla ya mavuno; nami nimenyesha mvua juu ya mji mmoja, nikaizuia mvua isinyeshe juu ya mji mwingine; sehemu moja ilipata mvua, na sehemu isiyopata mvua ilikatika. Basi kutoka miji miwili mitatu walitanga-tanga kuendea mji mwingine wapate kunywa maji, wasipate ya kuwatosha; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.” 

2. Usilitaje bure Jina la Yesu ambaye huna uhusiano naye

Matendo ya Mitume 19:13,15,16 “Baadhi ya Wayahudi wenye kutanga-tanga, nao ni wapunga pepo, wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nawaapisha kwa Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo. Yule pepo mchafu akawajibu, akawaambia, Yesu namjua na Paulo namfahamu, lakini ninyi ni nani? Na yule mtu aliyepagawa na pepo mchafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.”

3. Omba upewe roho iliyotulia (steadfast spirit) – roho ya kuwa na msimamo katika kusudi bila kuyumbayumba – uwe reliable, dependable.


Zaburi 51:10 “Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu.”

Maombi ya wiki hii:

1. Ee Mungu naomba uondoe ndani yangu roho ya kutangatanga kiroho, kiakili na kimaisha.

2. Ee Mungu naomba unipe moyo safi na roho iliyotulia ndani yangu.