WOKOVU WA KWELI NI ZAIDI YA SALA YA TOBA (Bofya hapa uangalie video)
WOKOVU
WA KWELI NI ZAIDI YA SALA YA TOBA
Ndoto: Nimeona watu wengi wakichoka kusubiri na kuamua
kuondoka kabla ya kupokea kile walichokuwa wameitiwa. Wengine walipoona wenzao
wanaondoka waliwafuata bila hata kujiuliza kwanini wanafanya hivyo.
Ebr 2:3 “sisi je!
Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa
na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia.”
Maeneo
ambayo tunahitaji kuokolewa
1.
Kuokolewa na dhambi: Wakolosai 1:13 “Naye alituokoa katika nguvu za
giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake.”
2.
Kuokolewa na dunia hii mbovu: Wagalatia 1:4 “ambaye
alijitoa nafsi yake kwa ajili ya dhambi zetu, ili atuokoe na dunia hii mbovu
iliyopo sasa, kama alivyopenda Mungu, Baba yetu.”
3.
Kuokolewa na ghadhabu itakayokuja: 1 Wathesalonike 1:10 “na
kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye alimfufua katika wafu, naye ni Yesu,
mwenye kutuokoa na ghadhabu itakayokuja.”
Tito ameeleza kwa muhtasari: Tito
2:11-14 “Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa
ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa,
katika ulimwengu huu wa sasa; tukilitazamia tumaini lenye baraka na
mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; ambaye alijitoa
nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi
katika matendo mema.”
Tufanyeje
ili tuwe salama?
1. Tuvumilie hata mwisho
Mathayo 10:22 “Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa
ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.”
Yakobo 5:11 “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri.
Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana
ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.”
2. Baada ya kuokolewa tunatakiwa KUSHINDA na sio kubweteka
Ufunuo wa Yohana 3:4,5 “Lakini unayo majina machache katika
Sardi, watu wasioyatia mavazi yao uchafu. Nao watakwenda pamoja nami hali
wamevaa mavazi meupe, kwa kuwa wamestahili. Yeye ashindaye atavikwa hivyo
mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina
lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba
yangu, na mbele ya malaika zake.”
Achana na imani potofu kwamba ONCE SAVED, ALWAYS SAVED.
Maombi
ya wiki hii:
1. Ee Mungu naomba unisaidie nishinde dhambi badala ya
kujifariji na sala ya toba wakati sina matendo mema.
2. Ee Mungu naomba uniwezeshe kuvumilia hata mwisho nisije
nikakosa uliyoniandalia kwa kuchoka kusubiri.
Lawi Mshana, 0712-924234 (ushauri na maombezi kwa njia ya mtandao).