Ticker

6/recent/ticker-posts

USIONE AIBU KUMFICHUA SHETANI ANAVYOKUTESA (Ujumbe wa video wenye maombezi)

USIONE AIBU KUMFICHUA SHETANI ANAVYOKUTESA (Bofya hapa uangalie video)

USIONE AIBU KUMFICHUA SHETANI ANAVYOKUTESA

Utangulizi: Shetani ana mbinu nyingi za kutesa watu. Kuna watu amewapa aibu waogope kuweka wazi matatizo yao ili shetani aendelee kuwakandamiza. Unapoona aibu kumwambia daktari tatizo lako unaliongeza zaidi au kukosa ufumbuzi wa kudumu.

Kilichomleta Yesu duniani ni kuharibu kazi za ibilisi. 1 Yohana 3:8 “atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.”

Mtume Paulo hakuficha tatizo alilopata kutokana na shetani

1 Wathesalonike 2:18 “Kwa hiyo tulitaka kuja kwenu, naam, mimi Paulo, mara ya kwanza, na mara ya pili, na Shetani akatuzuia.”

Hatumshindi shetani kwa kwenda kichwakichwa. 2 Wakorintho 2:11 “Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.”

2 Wakorintho 12:7 “Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi.”

Yesu alipojaribiwa nyikani, alimkemea shetani kwa kumpa sababu (kujibu hoja yake). Mt 4:9-11 “akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia.”

Maombi ya wiki hii:

1. Natangaza kila eneo la maisha yangu linalotawaliwa na shetani liachiliwe huru katika Jina la Yesu.

2. Napokea ukombozi kamili kutoka katika aibu ya kugonga milango na kubip na kupiga simu mara kwa mara za kuomba msaada wa kifedha katika Jina la Yesu. 

3. Ee Bwana nifungue kutoka katika taabu ya kazi zisizo na faida na shughuli zinazochanganya kichwa changu katika Jina la Yesu. 

4. Ee Mungu naomba unilinde dhidi ya udanganyifu wa kunitapeli nilichotaabikia katika Jina la Yesu.