Ticker

6/recent/ticker-posts

BARIKIWA KWA KUWASAIDIA WATU WASIOWEZA KUKULIPA


BARIKIWA KWA KUWASAIDIA WATU WASIOWEZA KUKULIPA

Tunashukuru sana kwa zawadi ya nguo kutoka kwenye familia ya Muheza, Tanga kwa ajili ya watu wanaoishi mazingira hatarishi wanaopokea misaada kupitia kwetu. Tuzidi kuwa na utamaduni wa kusaidia wasiojiweza badala ya kuwaachia watu wagombanie masanduku yetu ya nguo baada kuondoka kwetu duniani. Kuna mtu anahitaji sana vitu vyako ambavyo kwa sasa huvitumii.

Unaposaidia watu ambao pengine hawastahili upendo wako na hakuna hata siku moja watakushukuru kwa vile hawakujui, utapata thawabu kubwa mbinguni.

Luka 6:35 “Bali wapendeni adui zenu, tendeni mema, na kukopesha msitumaini kupata malipo, na thawabu yenu itakuwa nyingi; nanyi mtakuwa wana wa Aliye juu, kwa kuwa yeye ni mwema kwa wasiomshukuru, na waovu.”

Karibu sana uungane nasi katika utumishi huu usio na mipaka ya kidini wala kiitikadi.

Tunapokea misaada hii kutoka mahali popote ulipo.

Dr. Lawi Mshana, 0712-924234 (Simu na Whatsapp)