Ticker

6/recent/ticker-posts

TULIMALIZA SALAMA HUDUMA YA BURUNDI. NIKAGUNDUA KWANINI MUNGU ALINIPA FURSA YA KUSOMA LUGHA YA KIFARASA MIAKA ILIYOPITA.




TULIMALIZA SALAMA HUDUMA YA BURUNDI. NIKAGUNDUA KWANINI MUNGU ALINIPA FURSA YA KUSOMA LUGHA YA KIFARASA MIAKA ILIYOPITA.

Namshukuru sana Mungu kwa namna alivyoonekana kipekee katika huduma ya Burundi. Watu waliweke pembeni tofauti zao za kimadhehebu. Lakini pia nilifurahia sana ukarimu wa Warundi. Kila kanisa wamama wanakuwa na huduma ya kipekee sana. Hawakumsahau mke wangu hivyo walinikabidhi zawadi yake wakitambua kwamba huduma hii haingefika popote bila usaidizi wake.

Nilikutana na watu wengi ambao hawajui Kiswahili wala Kingereza isipokuwa wanajua Kirundi na Kifaransa. Hivyo sikupata shida kwa vile nilisoma hii lugha kwa miaka minne hapa kwetu Tanzania ingawa ni miaka mingi iliyopita. Nimegundua kwa nini nimekuwa nikipokea mialiko kutoka nchi zinazozungumza Kifaransa. Mungu anataka kutumia kila alichotujalia kuwa nacho kwa utukufu Wake.

Nawashukuru wote mliohusika katika umisheni huu. Naomba usichoke kutenda mema kwani utavuna kwa wakati wake. Wagalatia 6:9 “Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.”

Kama tulivyokusudia kuzifikia nchi mbalimbali tukianzia na hizi tunazopakana nazo, nimeona Mungu akifungua milango. Alikuwepo mchungaji kutoka Uganda. Naye ameomba huduma hii iwafikie waumini na wachungaji wa huko.

Tutakaposhirikishana kuchangia huduma hiyo naomba tuitikie tena kwa vile tunajiwekea akiba mbinguni kusiko na wezi wala kutu. Kumbuka vitu vingi tulivyo navyo hapa duniani, siku tukiondoka wengine watagawana na tutasahaulika. Mathayo 6:20 “bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi.”

Neema ya Mungu iwe nawe daima.

Dr. Lawi Mshana, Korogwe, Tanga, Tanzania; +255712924234